Meneja Alan Pardew ameeleza Nyota
huyo atakosa michezo mitano ya ligi kuu, na anatarajiwa kurejea dimbani
katikati ya Mwezi Januari 2015
Newcastle itamtumia mlinda mlango
wake wa pili Rob Elliott kuziba pengo la Tim Krul mpaka katikati ya januari
ambako inatazamiwa atakua kapona.
Alan Pardew bado pia anawasiwasi
na hali ya mlinzi wake mwenye majeruhi Daryl Janmaat aliyeumia kwenye mchezo
dhidi ya West Ham katika dimba la Upton Park.
Newcastle itaendelea kuwakosa
mshambuliaji Siem de Jong, viungo Ryan Taylor, Rolando Aarons, Mehdi Abeid na
mabeki Fabricio
Coloccini and Davide
Santon.walioko nje kwa majeruhi huku viungo Moussa Sissoko na Jack Colback
wakiendelea kutumikia adhabu zao.
Post a Comment